Mama wa mmiliki Alliance afariki siku ya kumuaga mwanaye

 

Nchagwa Manga, mama mzazi wa Mkurugenzi

wa Kituo cha Michezo cha Alliance kilichopo jijini Mwanza, James

Bwire aliyefariki Januari 25, 2025, naye amefariki leo ljumaa Januari

31, siku ya kumuaga mwanaye

Akizungumza na Mwananchi leo ljumaa Januari 31, 2025,

Mwenyekiti wa Kituo cha Alliance, Stephano Nyaitati amethibitisha

kifo cha Nangwa

Nyaitati amesema kikongwe huyo amefariki asubuhi ya leo (ljumaa)

wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ye

Bugando, saa chache kabla ya kufanyika ibada ya kuagwa mwili wa

mtoto wake

Bwire alifariki Januari 25, 2025 saa 4 usiku wakati akipatiwa

matibabu katika Hospitali hiyohiyo ya Bugando, Mwanza baada ya

kuugua ugonjwa wa kiharusi kwa muda mrefu.

Licha ya kutokea kwa msiba wa kikongwe huyo, Nyaitati amesema

ratiba ya kumuaga na kumzika James Bwire, itaendelea kutekelezwa

<ama ilivyopangwa, kisha itaandaliwa ratiba nyingine kwa ajili yə

mazishi ya mama yake

Post a Comment

0 Comments