I phone Zinaweza kupata intaneti ya satelaiti bila kutegemea mitandao ya simu



 Apple inaripotiwa kushirikiana na SpaceX kuunganisha

huduma za internet za satelaiti za Starlink kwenda moja

kwa moja kwenye iPhones. Watumiaji wa iPhone wataweze

kupata internet bila huduma ya mtandao wa simu

Kipengele hiki, kimeanza kufanyiwa majaribio katika

mfumo mpya wa ioS 18.3, kwa sasa utaratibu huu

unafanyika kama majaribio kwa watumiaji wachache wa

T-Mobile nchini Marekani

Mfumo huu utafanya kazi kiotomatiki pale mtumiaji akiwa

katika eneo ambalo hakuna mtandao lakini miaka ijayo

itakuwa ni huduma ya kawaida, hivyo watumiaji wa simu

wataweza kuamua kutumia mtandao wa Satelaiti au

mitandao ya simu.

Kwa sasa tayari watumiaji wa iPhone wanaweza kupata

nuduma za dharura kama vile kutuma meseji, kupiga simu

na kutafuta kifaa kilichopotea; lakini soon internet itakuwa

kwenye option

Unaonaje teknolojia hii?

Post a Comment

0 Comments